Offline
Menu
BOMOA MADHABAHU ZA GIZA ZINAZOFUATILIA NDOA YAKO ILI KUHARIBU NA KUBOMOA
By CRISPIN ADAM
Published on 09/26/2025 15:51
News

MWONGOZO   WA  MAOMBI   JUU  YA  MISINGI   YA NDOA  .

 

OMBI  KUU:  BOMOA  MADHABAHU   ZA GIZA   ZINAZOFUATILIA  NDOA  YAKO  ILI  KUHARIBU   NA  KUBOMOA .

 

Mungu  anakaa  kwenye  madhabahu na  shetani  naye  anakaa  kwenye  madhabahu,Kwenye  madhababu  kuna  roho   ambazo  huwa  zinaitumikia  madhababu ,ni roho   zilizo  wahudumu   wa madhabahu  hizo,Na kwenye   madhababu   ndipo  zinapokaa roho   za  watu  pia.

 

Maisha  ya  mwanadamu   kama  hayapo  kwenye  madhababu  ya  Mungu  basi  yapo  kwenye  madhababu  ya  Shetani  na  Hiki ndicho kilichomleta  Yesu  ,KUJA  KUMKOMBOA  MWANADAMU  KUTOKA  HUKO  KWENYE  MADHABAHU   ZA GIZA.

 

Na  Mungu ni  Mwangalifu   sana ,UKIWA   NI  MTU  WAKE    CHA KWANZA  UKIWA  UNATEMBEA  NAYE ,ANASEMA NA  WEWE  KWANZA   NA KUKUPA  TAADHARI JUU  YA MADHABAHU    ZA  MIUNGU  MINGINE  KUWA  USIFANYE  NAO MAAGANO.

 

Kutoka 23:32 (KJV)  " Usifanye maagano pamoja nao, wala pamoja na miungu yao."

 

Kutoka 34:13

" Bali utabomoa madhabahu zao, na kuvunja-vunja nguzo zao, na kuyakata-kata maashera yao."

 

MAAGANO   NI  KITU  CHA  KIMADHABAHU.

 

NDIYO  SABABU  PIA NDOA  INAFUNGWA  MADHABAHUNI.

 

KWENYE  HIYO  MADHABABU  NDOA  INAPOFUNGWA  KUNA  MUNGU  AU  SHETANI.

 

KILA  MADHABAHU  INA  MUNGU  WAKE.

NDIYO  SABABU  KUNA MADHABAHU  ZA AINA  MBILI  KUU

 

1.MADHABAHU  TAKATIFU  YA  MUNGU  ALIYE  HAI

 

2.MADHABABU  YA  MASHETANI.

 

Kwenye  madhabahu  Yeyote  IMEBEBA  MFUMO   WA  MAISHA   WA  WATU  WALIOAMUA  KUMFUATA  MUNGU  WA  HIYO  MADHABAHU. 

 

MADHABAHU  IMEBEBA  (  ROHO   ZA  WATU/MAAGANO/ROHO/ MANENO/SAUTI/MUNGU  AU  MIUNGU/SADAKA N.K)  KWA  KIFUPI  NI KUWA  MADHABABU  INATOA  MFUMO   WA  MAISHA ( LIFE STAILY)   KWA  WATU  WA ENEO   HUSIKA  WANAOISHI  KWENYE    ENEO  HUSIKA  AU  FAMILIA  HUSIKA  ,MAANA  ULIANZA  KUONGELEA  JUU YA  MADHABAHU   ZIPO  ZA  KIFAMILIA/KIMTAA/KIMKOA/KIKANDA/KITAIFA/KIMATAIFA .NK

 

SASA  KUNA  WATU  AMBAO  MADHABAHU  ZINAWEZA   KUWAKATALIA  KWA HABARI  YA  KUWA NA    NDOA  AU  KUNA  WATU AMBAO MADHABAHU  ZAKO  ZINAWEZA  KUWASHIKILIA NA  ZISIWAACHIE  KABISA  HATA  WAKIOLEWA  WANAENDA  KWENYE NDOA NA  MADHABAHU  ZAO NA  MIUNGU  YAO,HAPO NDIYO INAKUWA KAZI KWELI KWELI.

 

MFANO:  1

 

YAKOBO  ALIPOMCHUKUA  LEA NA RAHELI  KAMA  WAKE  ZAKE ,WAKE   ZAKE  HAWA  HAWAKUIACHA  MIUNGU  YA BABA  YAO ,WALIKUJA NAYO KWENYE   MAISHA MAPYA  YA NDOA  YA  NDUGU  YETU YAKOBO,YAKOBO  AKAWA ANAFUATILIWA SANA NA  LABANI NA  VITA  VIKAWA  VIKUMBWA ,HAKUJUA  KUWA  HUKO  ALIPOOA  WALE  MABINTI   WANAABUDU  MIUNGU  NA YAKOBO  HAJUI.

 

Mwanzo 31:30

" Basi sasa, umetoka kwa sababu umetamani sana nyumba ya baba yako. Mbona basi umeiiba miungu yangu?"

 

Mwanzo 35:2

 "Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake, na wote waliokuwa pamoja naye, Ondoeni miungu migeni iliyoko kwenu, mjisafishe mkabadili nguo zenu."

 

Mwanzo 35:4

" Nao wakampa Yakobo miungu migeni yote iliyokuwa mikononi mwao, na pete zilizokuwa masikioni mwao, naye Yakobo akazificha chini ya mwaloni ulioko Shekemu."

 

Yakobo   alioa  Familia ambayo  MABINTI   WALIONDOKA NA MIUNGU  YA  BABA  YAO  NA  KWENDA  KUANZA  FAMILIA  MPYA  ,MAANA  YAKE  MISINGI  YA  FAMILIA  HII  ILIKUWA  MIBOVU  KABISA.

 

●Wewe  haujawahi  kuona  mtu  anaolewa  lakini  ANAINGIA  KWENYE  NDOA NA MATAMBIKO  KIBAO  NA KAFARA  KIBAO   KAFANYIWA  ILI AKADUMU  KWENYE NDOA,USHIRIKINA  UMEFANYWA  HASWA.

●WEWE  HAUJAWAHI  KUONA  MTU ANAOLEWA ANAKUJA NA TARATIBU  ZA  KWAO  ZA KIMILA  KUJA  KUMRUBUNI  MWEZI   WAKE NAYE  AZIFUATE

●KUNA  WATU  WANAOA/KUOLEWA WANAKUJA NA  ZANA  ZA  KISHIRIKINA  HAUJAWAHI  KUONA NAKUAMBIA,HATA  NYUMBA  WANAYOIISHI  LAZIMA  IZINDIKWE  VILIVYO.

 

MFANO :  2

 

BINTI   ALIYE OLEWA NA  WANAUME  SABA NA  WOTE  WAK

 

Madhabahu  ya  kwao HAWA  VIJANA   haikutana  Huyu  Binti  awe na  ndoa  ,NA  HII  FAMILIA  MADHABAHU  YAKE  ILIUA  WATOTO  WOTE   SABA  WA KIUME WALIO OA HUYU  BINTI  ,Watu  wakamfuata  Yesu  wakamueleza habari   za  huyu  binti.

 

Mathayo 22:25-27 (KJV)  " Basi, kwetu kulikuwa na ndugu saba; wa kwanza akaoa, akafariki, na kwa kuwa hana mzao, akamwachia nduguye mke wake.

 Vivyo hivyo wa pili naye, na wa tatu, hata wote saba.

 Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye."

 

●Kila  akioa  mke  anakufa

 

●Kila akiolewa  anakufa

●Kila  akiolewa  anaachika  ( Kuna  familia   za hivi  ujue)

●Kila  akiolewa ,ataolewa ila  hazai watoto

●Kila  akioa   wanawake   hawakai,kila  siku  anakuwa  ni  wa kuoa   tu  na  kuacha

●Baada ya  kuoa  tu,AKAFILISIKA

●BAADA YA  KUOA  AKAFUKUZWA KAZI

●MWINGINE   KAOA  ILA  KILA  MAHALI ANA  WANAWAKAE     WA KUTOSHA  AU  WANAUME ( ukifuatilia   kwao ndivyo   walivyo)

●Wengine  tangu  waingie kwenye  ndoa  Hakuna   wanachofanya     wakafanikiwa

●Wengine   hawaoi

●Wengine  hawaolewi

 

KUNA MAMBO MENGI   SANA  KWENYE  MAISHA YA   WATU,WATU  WANAPITIA  MENGI ,NA  WENGI  HAWASEMI  ILA  WANATESEKA  SANA  KWENYE  NDOA, WENGINE  WANAFIKIRI  "NI  TABIA  YA  MTU"  VINGINE  SI  TABIA NI  UNAPAMBANA NA MADHABAHU  ZA  FAMILIA  ZA  WATU,UMEOA   AU KUOLEWA  KWENYE  FAMILIA  ULIYODHANI  UNAIJUA  KUMBE  HUIJUI.....UNAFIKIRI  UNAPAMBANA NA TABIA  KUWA  MWENZAKO  KABADILIKA..SI KABADILIKA BALI  MAISHA  YAKE  YAMEFUGWA  KWENYE  MADHABAHU  ZA  FAMILIA NA  UKOO   WAKE,NA  ANAYETESEKA NI  WEWE.

 

YAKOBO  ALIPAMBA  NA  ALIKUJA    KUJUA  BAADAYE   SANA KUWA  ALIPOOA  WANATEGEMEA  MIUNGU KUFANIKISHA MAMBO  YAO.

 

 

 

●MUONGOZO WA MAOMBI YA KUKATAA ROHO YA UHARIBIFU KWENYE FAMILIA YAKO

 

“Kama misingi ikiharibika,

Mwenye haki atafanya nini?” Zaburi 11:3

 

“Na watu wako watapajenga mahali palipokuwa ukiwa; utaiinua misingi ya vizazi vingi; nawe utaitwa, Mwenye kutengeneza mahali palipobomoka; na, Mwenye kurejeza njia za kukalia.” Isaya 58:12

 

●MAOMBI 

 

I. Baba katika jina la Yesu,asante kwa neema yako na baraka zako kwangu na familia yangu.

 

II. Nimesimama mbele zako eeh Yesu ,kuomba rehema na toba juu ya familia yangu.

 

●TOBA KWENYE MISINGI YA FAMILIA YA YAKO.

 

2 Nya 7:14 (SUV)

....  “ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.”

 

III. Ninaomba rehema zako kwenye misingi ya familia yangu eeh Yesu.

 

IV. Ikiwa kuna misingi mibovu ninayunyiza damu ya Yesu kwenye misingi ya familia yangu.

 

V. Ikiwa kuna maagano au matambiko yalifanyika na yakampa adui uhalali wa kuishambulia familia yangu,ninaomba rehema na toba mbele zako eeh Bwana.

 

VI. Ikiwa kwenye familia kuna mtu anaendelea kuabudu miungu au kuitegemea kwa siri ,ninaomba rehema juu yake eeh Yesu.

 

VII. Ninakataa kila roho za giza zinazoitawala familia yangu kwa jina la Yesu.

 

VIII. Ninanyunyiza damu ya Yesu juu ya kila nafsi ya mwanafamilia kwa jina la Yesu.

 

IX. Ninaondoa kila laana na matamko ya kipepo kwenye familia yangu kwa jina la Yesu.

 

●VUNJA KILA MADHABAHU YA GIZA KWENYE FAMILIA NA MISINGI YAKE

 

“Vunjeni kabisa mahali pote walipokuwa wakiitumikia miungu yao mataifa mtakayoyamiliki, juu ya milima mirefu, na juu ya vilima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi;

nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za miungu yao zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo.” Kumbukumbu 12:2-3

 

X. Baba katika jina la Yesu,ninakata kila madhabahu ya giza  kwenye familia yangu.

XI. Ninafunga kila nguvu za giza kwenye familia yangu ,kwa jina la Yesu.

XII. Ninafunga kila roho za giza zilizokuwa zinatumika kuharibu familia yangu kwa jina la Yesu.

 

XIII. Ninateketeza kila mipango ya siri ya uharibifu iliyotengenezwa na madhabahu za giza juu ya familia yangu kwa jina la Yesu.

 

XIV. Ninafuta kila kafara au sadaka za giza kwenye familia yangu ,Kwa damu ya Yesu.

 

XV. Ninatakasa ardhi na anga la familia yangu ,kwa jina la Yesu.

 

XVI. Ninafuta majina na kazi za wana familia kwenye madhabahu za giza kwa Jina la Yesu.

 

XVII. Ninaondoa kila muunganiko wa kipepo uliokuwepo kwa jina la Yesu.

 

XVIII. Ninangusha  kila mfumo wa utendaji kazi wa giza na madhabahu hizo kwa jina la Yesu.

 

●ONDOA KILA MAUTI NA UHARIBUFU KWENYE FAMILIA YAKO

 

.....  “mauti imemezwa kwa kushinda.” 1Wakoritho 15:54

 

XIX. Baba katika jina la Yesu  ninaipinga mauti na uharibifu kwenye familia yangu ,kwa jina la Yesu

 

XX. Kila mauti iliyojificha kwa siri ,ninaing`oa kwa jina la Yesu.

 

XXI. Kila mpango wa kuzimu juu ya familia yangu,ninauondoa kwa jina la Yesu.

 

XXII. Kila uharibifu ninaupinga kwa jina la Yesu.

 

XXIII. Ninakataa magonjwa,wivu mbaya kwa jina la Yesu.

 

XXIV. Ninazipinga ajali na kila roho ya kupoteza au kuibiwa na maonevu ya kila namna  kwa jina la Yesu.

 

XXV. Kila mateso na yakome kwa jina la Yesu.

 

XXVI. Roho ya hofu,woga naikataa kwenye familia kwa jina la Yesu.

 

XXVII. Kila roho ya vurugu na kukosa furaha ninaiondoa kwa jina la Yesu.

 

●TAMKA BARAKA KWENYE FAMILIA

 

Ebr 6:14 (SUV)

...  “akisema, Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza.”

 

XXVIII. Baba katika jina la Yesu,ninaomba ile roho ya baraka na iwe kwenye familia yangu.

 

XXIX. Ile nguvu ya uwezeshi na ije kwenye familia yangu kwa jina la Yesu.

 

XXX. Baraka kwenye afya,Uchumi,amani kwenye kila eneo kwa jina la Yesu.

 

XXXI. Ninatamka uponyaji ,kufunguliwa kwenye kila eneo kwa wanafamilia kwa kwa jina la Yesu.

 

XXXII. Ninatamka Mafanikio,neema,kuongezeka,kustawi kwenye kila jambo na kwenye kila eneo kwa jina la Yesu

 

XXXIII. Baraka ya kiagano ya ulinzi wako juu ya familia ikawe juu ya familia yangu kwa jina la Yesu.

 

Crispin Adam UKUTA WA MAOMBI WhatsApp 0754 56 64 05 AU 0682 94 9191 

UKUTA WA MAOMBI-KWA ZOO BUYUNI CHANIKA

Comments
Comment sent successfully!